SIMBA, YANGA KUPEPERUSHA BENDERA KIMATAIFA

Timu za Simba na Yanga zinazoshiriki mashindano ya kimataifa wikiendi hii zinaingia uwanjani kuanza safari ya kutafuta ubingwa wa kombe la klabu Bingwa Afrika na kombe la Shirikisho katika michezo ya makundi mzunguko wa kwanza.

Simba wawakilishi katika klabu Bingwa Afrika leo watakuwa ugenini katika nchi ya Guinea dhidi ya timu ya Horoya AC mechi itakayoanza majira ya 01:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki kwenye uwanja wa General Lansana Conte.

Huu ni mchezo wa pili katika kundi la Simba baada ya hapo jana timu ya Raja Casablanca ya Morocco ikiwa uwanja wa nyumbani kuanza kwa kuifunga Vipers ya Uganda mabao 5-0.

Timu ya Yanga itaanza ushiriki wake katika kombe la Shirikisho nchini Tunisia kesho katika mchezo dhidi ya timu ya US Monastir majira ya 01:00 usiku kwenye uwanja wa Olympic Rades jijini Tunis.

Timu ya Yanga iliyo katika kundi moja na TP Mazembe, Monastir na Real Bamako imefanikiwa kuingia hatua ya makundi mwaka huu katika mashindano ya kimataifa ikiwa ni baada ya miaka mitano.

Baada ya michezo hiyo ya kimataifa timu hizo zitarejea kuendelea na michezo ya Ligi Kuu ya NBC, Simba itacheza dhidi ya Azam katika uwanja wa Mkapa, Dar ikiwa ni ‘Mzizima derby’ Februari 21 na Yanga itakua ugenini dhidi ya KMC Februari 22 katika uwanja wa Mkapa, Dar.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *