YANGA YAONGEZA NAMBA KATIKA HISTORIA

TIMU ya Yanga imekabidhiwa ubingwa wa Ligi Kuu ya NBC kwa mara ya 29 ikiwa ni mara saba zaidi ya timu inayofuatia ya Simba iliyotwaa mara 22 na mara ya pili mfululizo tangu Ligi hiyo ianze kudhaminiwa na Benki ya NBC.

Fiston Mayele na Yanick Bangala wamehitimisha msimu kwa ‘Wananchi’ wakifunga mabao mawili yaliyoipa ushindi timu hiyo dhidi ya Prisons ya Mbeya kwenye uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.

Huu ni mojawapo ya msimu bora kwa timu ya Yanga ikimaliza kwa kushinda mechi nyingi kuliko timu yeyote (25 ) , kutoa sare mitatu, kupoteza miwili na kukusanya alama 78 wakiwazidi watani zao wa jadi Simba kwa alama tano.

Timu hiyo inaelekea mkoani Tanga itakapocheza na timu ya Azam iliyomaliza msimu kwa kuifunga Polisi Tanzania ya mkoani Kilimanjaro mabao 8-0 kwenye mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam Juni 12 katika uwanja wa Mkwakwani.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *