DODOMA, MTIBWA HAKUNA MBABE

Mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Dodoma Jiji na Mtibwa Sugar uliochezwa katika uwanja wa Jamhuri, Dodoma umemalizika kwa sare ya bao moja.

Bao la Mtibwa Sugar lilifungwa na Abdul Hilary dakika ya 18 huku la Dodoma Jiji likifungwa na Emmanuel Martin dakika ya 38.

Dakika ya 25 mchezo ulilazimika kusimama baada ya golikipa wa Mtibwa Sugar Mohammed Makaka kudondoka ghafla na kuwahishwa hospitali.

akizungumza na Azam Tv baada ya mchezo kumalizika daktari wa Mtibwa Laurence Mushi amesema hali ya Makaka inaendelea vizuri kwasasa kinachosubiriwa ni majibu ya vipimo kujua nini Tatizo.

“Alianguka ghafla pasipokua na mpira wowote wa kugombania, baada ya kumuangalia nikagundua amepoteza fahamu tukamuwahisha hospitali, kwasasa anaendelea vizuri lakini tunasubiri majibu ya vipimo vya hospitali “ alisema Mushi

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *