NYOTA LIGI KUU YA NBC WANG’ARA AFCON 23.

 

MICHUANO ya fainali za mataifa ya Afrika 2023 zinaendelea nchini Ivory Coast katika miji ya Abdijan, korhogo, Bouake, Yamoussoukro na San Pedro.

Michuano hii inajumuisha nyota 18 kutoka timu tano zinazoshiriki Ligi Kuu ya NBC.

Stephane Aziz Ki na Djigui Diarra ndiyo wachezaji wa kwanza kuiwakilisha Ligi Kuu ya NBC kwenye Fainali hizi za 2023 ambapo waliyawakilisha mataifa yao ya Burkina Faso kwa Ki na Mali kwa Diarra kupata ushindi kwenye michezo yao ya kwanza.

Nyota wengine 16 leo wanatarajiwa kuyawakilisha mataifa yao kwenye michezo ya kwanza kwenye fainali hizo ambapo Zambia, Dr Congo na Tanzania zitaanza kutupa karata zao hii leo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *