LIGI ya NBC Championship inaendelea leo kwa michezo mitatu ya mzunguko wa 25 kupigwa leo.
Mkoani Mtwara Mbeya Kwanza itakuwa mwenyeji wa Stand United saa 8:00 mchana kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona huku Mbeya Kwanza ikiwa nafasi ya nne kwenye msimamo ikiwa na alama 47 kwenye michezo 24.
Saa 10:00 alasiri Pamba itakuwa mwenyeji wa Mbeya City kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza.
Pamba imejikusanyia alama 51 kwenye michezo 24 ikiwa nafasi ya pili huku Mbeya City ikiwa nafasi ya saba na alama 38.
Mchezo wa mwisho utazikutanisha Polisi Tanzania dhidi ya TMA kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha saa 10:00 alasiri.
Michezo hii ya Ligi ya NBC Championship itaoneshwa mubashara kupitia chaneli ya TV3 na ST Bongo kwenye king’amuzi cha Startimes.