LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo kwa mchezo mmoja wa Ligi Kuu ya NBC Kati ya Azam na Yanga saa 2:30 usiku kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.
Azam inaingia kwenye mchezo huu unaotambulika kama ‘Dar es Salaam Derby’ ikiwa nafasi ya tatu na alama 44 baada ya michezo 20 huku Yanga ikiwa nafasi ya kwanza na alama 52 kwenye michezo 19.
Azam inahitaji kushinda mchezo huu ili kupunguza tofauti ya alama na Yanga na kuendeleza mbio za ubingwa huku Yanga ikihitaji kujikita kileleni mwa msimamo na kuongeza utofauti wa alama na timu zinazofuata.
Yanga inaongoza kwa ufungaji wa mabao ikifunga 48 kwenye michezo 19 na kuruhusu mabao tisa pekee huku Azam ikifuata kwa upachikaji wa mabao ikifunga 45 na kuruhusu 15.
Mchezo huu utakuwa wa mwisho kupisha michezo ya kalenda ya kimataifa ya FIFA kwa timu za taifa kabla ya kurejea tena Aprili 12, 2024.