COASTAL UNION YASHINDWA KUFURUKUTA IKIWA NYUMBANI

LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja kati ya Coastal union na JKT Tanzania kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga na kushuhudia Coastal Union ikishindwa kutamba baada ya kufungwa mabao 1-2.

Mchezo ulianza kwa kasi na ilikuwa Coastal Union iliyokuwa ya kwanza kuandika bao dakika ya 21 kwa shuti kali la mchezaji Athumani Makambo.

Bao hilo lilidumu kwa dakika 14 pekee kabla ya Saleh Karabaka kuisawazishia JKT baada ya kupokea pasi kutoka kwa Mohamed Bakari.

Kipindi cha pili JKT ilibadilisha mchezo na dakika ya 67 kuongeza bao la pili lililofungwa na Mohamed Bakari aliyekuwa na siku nzuri ‘kazini’ baada ya makosa ya kiulinzi yaliyofanywa na mabeki wa Coastal Union.

Katika mchezo huo Ally Msengi wa JKT aliibuka mchezaji bora wa Mchezo huo baada ya kufanya kazi kubwa ya kiulinzi iliyowapa alama tatu ‘maafande’ hao.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *