KIUNGO wa Azam Feisal Salum ameendelea kuwa kinara wa kutoa Pasi za mabao katika Ligi Kuu ya NBC akiwa na Pasi 13 katika mechi 11 alizocheza msimu huu hadi sasa.
Pacome Zouzoa wa Yanga anashika nafasi ya pili akiwa na Pasi 9 huku akifuatiwa na wachezaji wenzake Maxi Nzengeli wa Yanga na Prince Dube wenye pasi 8 za mabao sawa na kiungo wa Singida Black Stars.
Kiungo Jean Ahoua wa Simba na Stephane Azizi Ki wa Yanga wanafuata wakiwa na Pasi 7 kila mmoja ikisalia mizunguko mitatu msimu kutamatika huku baadhi ya timu zikiwa na michezo ya ‘kiporo’.