HAUSUNG, RHINO VINARA MBIO ZA KUPANDA LIGI YA CHAMPIONSHIP YA NBC.

LIGI ya First League inazidi kupamba moto kwenye viwanja tofauti huku timu za Hausang ya Makambako Njombe na Rhino Rangers ya Tabora zikiongoza mbio hizo.

Timu ya Hausang inaongoza kundi A baada ya kucheza michezo 12 ikishinda michezo sita, sare nne na kupoteza miwili huku ikifanikiwa kukusanya alama 22.

Timu ya Magnet inashika nafasi ya mwisho kwenye msimamo wa kundi hilo ikiwa na alama 11 baada ya kushinda michezo miwili, kupoteza mitano na sare tano.

Rhino Rangers inashikilia usukani wa kundi B ikikusanya alama 28 baada ya kushinda michezo tisa, sare mchezo mmoja na kupoteza michezo miwili.

Rhino inaongoza pia kwenye kupachika mabao ikifunga (30) huku Ruvu Shooting ikiwa timu iliyofunga mabao machache hadi sasa ikifunga mawili pekee.

Kinara wa kundi A atakutana na kinara wa kundi B katika mchezo wa mwisho wa msimu ili kumpata bingwa wa Ligi ya First League msimu wa 2024/25.

One comment

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *