LIGI ya championship ya NBC inazidi kushika kasi ikielekea ukingoni huku Mbeya City ikiwa kinara wa ‘kupachika’ mabao baada ya kufunga mabao 45 hadi sasa ikiwa ni idadi kubwa kwa timu ya Ligi hiyo hadi sasa.
Mbeya city ipo nafasi ya pili kwenye msimamo ikiwa na alama 49 huku Mtibwa sugar ikiwa kinara kwenye msimamo na alama 54 na ikishika nafasi ya pili kwa mabao baada ya kufunga 44 na kuruhusu mabao 11 hadi sasa.
Geita gold inashika nafasi ya nne kwenye msimamo ikiwa na alama 48 huku ikiwa timu ya tatu kwa idadi kubwa ya mabao baada ya kufunga 41 huku ikifungwa mabao 17.
Stand united ni timu ya nne kwa kupachika mabao ikiwa nayo 37 na kufungwa 19 huku ikishika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi na alama 49.