MBEYA CITY WAKALI WA ‘KUTUPIA’ NBC CHAMPIONSHIP

TIMU ya Mbeya City imeendelea kuongoza kwa kufunga mabao kuliko timu yoyote katika Ligi ya Championship ya NBC licha ya kuwa katika nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi hiyo.

Mbeya City wamefanikiwa kufunga mabao 58 katika michezo 28 ambayo timu hiyo imecheza huku ikiwa imeruhusu mabao 26 na kukusanya alama 62 ikiwa nafasi ya pili katika msimamo nyuma ya Mtibwa Sugar ambayo imeshapanda Ligi Kuu ya NBC.

Mtibwa Sugar wanafuatia kwa kufunga mabao ikifunga mabao 54 na kuruhusu mabao 16 katika michezo 28 iliyocheza huku ikiwa imekusanya alama 67 na ikiongoza katika msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC.

Geita Gold imefanikiwa kufunga mabao 49 huku ikiruhusu mabao 24 pamoja na kuvuna alama 54 ikiwa nafasi ya nne katika msimamo huku Stand United ikifunga mabao 47 na kuruhusu  mabao 23 wote wakiwa  wamecheza michezo 28 katika Ligi hiyo.

Mbeya Kwanza imefunga mabao 40 baada ya kucheza michezo 28 ikiruhusu nyavu zake kutikiswa mara 26 na ikiwa nafasi  ya sita katika mbio za ubingwa wa Ligi hiyo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *