MTIBWA VS GEITA

MTIBWA, GEITA VITA YA UONGOZI NBC CHAMPIONSHIP.

JUMLA ya mechi tano (5) zinachezwa leo Februari 26, 2025 kwenye mikoa ya Lindi, Pwani, Morogoro na Arusha huku michezo yote ikianza saa 10:00 alasiri.

Mchezo unaosubiriwa kwa hamu hii leo unazikutanisha Mtibwa Sugar dhidi ya Geita Gold kwenye uwanja wa Manungu mkoani Morogoro, Mtibwa inaongoza msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 48 huku Geita Gold ikishika nafasi ya pili ikiwa na alama 45.

Upekee wa mchezo huu ni kuwa yeyote anayeshinda anakaa kileleni mwa msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC, Mchezo wa Duru ya kwanza uliochezwa kwenye uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita, Geita Gold ilishinda kwa bao 1.

Mkoani Lindi Bigman FC itaialika Biashara United, Cosmopolitan itakuwa mwenyeji wa Kiluvya Jamhuri – Morogoro, kwenye uwanja wa Mabatini mkoani Pwani Transit Camp itawapokea Green warriors, mchezo wa mwisho kwa leo utazikutanisha Mbuni dhidi ya Mbeya City kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *