SIMBA VS AZAM

MZIZIMA ‘DERBY’ HAKUNA MBABE.

HAKUNA Mbabe ndivyo unavyoweza kusema baada ya mchezo wa ‘Derby’ ya mzizima kati ya Simba SC na Azam FC kutamatika kwa sare ya mabao 2-2 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.

Mabao ya Azam FC yamefungwa na Gibrill  Sillah na Zidane Sereri huku yale ya Simba SC yakifungwa na Elie Mpanzu na Abdulrazack Hamza.

Zidane Sereri wa Azam FC alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo, Zidane aliyecheza dakika 10 pekee alihusika kwenye bao la mwisho la Azam FC ambalo liliihakikishia Azam FC kupata alama moja kwenye mchezo huo.

Simba inendelea kusalia nafasi ya pili ikiwa na alama 51 baada ya michezo 20 wakati Azam FC ikiwa nafasi ya tatu ikiwa na alama 44 kwenye michezo 21 ya Ligi Kuu ya NBC.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *