Ligi ya Championship ya NBC mzunguko wa 24 umemalizika kwa Mtibwa Sugar kuwa kinara ikiwa na alama 57 na kushika nafasi ya kwanza huku ikifunga mabao 47 na kufungwa mabao 34.
Nafasi ya pili inashikwa na Mbeya City yenye alama 52 mabao 48 huku ikifuatiwa na Stand United inayoshika nafasi ya tatu na alama 52 ikifunga mabao 40.
Geita Gold inashika nafasi ya nne ikikusanya jumla ya alama 48 baada ya kufunga mabao 41 na kufungwa 22.
Timu hizi nne zipo kwenye ushindani mkubwa wa kugombea nafasi ya kucheza Ligi Kuu ya NBC msimu ujao zikipishana kwa tofauti ya alama chache kwenye msimamo.