DODOMA JIJI KUMALIZA ‘KIPORO’ CHA LADHA ZA LIGI KUU YA NBC KESHO.

LIGI Kuu ya NBC inatarajiwa kuendelea kesho kwa mchezo namba 148 ambapo timu ya Simba itaikaribisha timu  ya Dodoma jiji katika uwanja wa KMC Complex mkoani Dar es Salaam majira ya saa kumi jioni.

Simba ipo nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa  na alama 54 ikifunga mabao 46 na kuruhusu mabao 8 katika michezo 22 timu hiyo iliyocheza mpaka sasa.

Dodoma Jiji iko nafasi ya nane  kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya  NBC  huku ikiwa na alama 27 ikifunga mabao 22 na kuruhusu 27 katika michezo 22 iliyocheza mpaka sasa.

Mechi hiyo ya Simba na Dodoma Jiji iliahirishwa kutokana na ajali iliyopata timu ya Dodoma Jiji ikitokea Ruangwa mkoani Lindi  kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya  timu ya Namungo

 

 

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *