KIUNGO wa timu ya Simba Jean Ahoua ameendelea kujiimarisha kwenye mbio za ufungaji bora baada ya kufikisha mabao 15 ikiwa ni msimu wake wa kwanza tangu ajiunge na timu hiyo kwenye Ligi Kuu ya NBC.
Ahoua amefanikiwa kufunga mabao hayo akiwa amecheza mechi 24 kwa jumla ya dakika 1773 katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2024/2025.
Clement Mzize wa Young Africans anafuata akiwa amefanikiwa kufunga mabao 13 huku mchezaji mwenzake Prince Dube wa timu hiyo akifanikiwa kucheka na nyavu za wapinzani wao mara 12 sawa na Leonel Ateba wa Simba.
Steven Mukwala wa Simba na Jonathan Sowah wa Singida Black Stars wamefanikiwa kufunga mabao 11 kila mmoja huku Elvis Rupia wa Singida Black Stars akitupia nyavuni mabao 10.