Tag: Ligi Kuu

MASHUJAA, YANGA MILANGO MIGUMU

TIMU ya Mashujaa ya mkoani Kigoma na Yanga ya Dar zimetimiza michezo mitatu ya Ligi Kuu ya NBC bila kuruhusu bao lolote.

Yanga imecheza michezo mitatu nyumbani ikikusanya alama zote tisa na kuongoza msimamo wa ligi pasipo kuruhusu bao huku ikifunga mabao 11 ambapo tisa kati ya hayo yamefungwa kipindi cha pili.

Mashujaa iliyopanda daraja baada ya kuiondoa Mbeya City ya Mbeya kwenye michezo ya mtoano imeendelea kuonesha ubabe ikicheza michezo mitatu kwenye uwanja wa nyumbani bila kupoteza wala kufungwa bao huku ikiwa na alama saba katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi