LIGI Kuu ya NBC leo itaendelea mkoani Dar es Salaam katika viwanja viwili ambapo timu ya Simba itakuwa mwenyeji wa Mashujaa katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo majira ya saa 10:00 alasiri huku timu ya Azam ikiwaalika TRA katika uwanja wa Azam Complex Chamazi saa 1:00 usiku.
Simba ipo nafasi ya sita katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imecheza michezo sita, ikishinda michezo minne, sare moja na kufungwa mchezo mmoja huku ikikusanya alama 13.

Mashujaa ipo nafasi ya nane katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikicheza michezo 10, ikishinda michezo mitatu, sare nne na kufungwa michezo mitatu huku ikikusanya alama 13.
Kwa upande wa timu ya Azam imecheza michezo saba hadi sasa bila kupoteza ikishinda michezo mitatu na sare nne na kufanikiwa kukusanya alama 13 katika michezo hiyo.
Timu ya TRA United ipo nafasi ya tisa katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa imecheza michezo nane, ikishinda michezo mitatu, sare tatu na kufungwa michezo miwili huku ikikusanya alama 12.