TIMU ya Tabora United imefanikiwa kuifunga timu ya Pamba Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliochezwa jana kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.
Tabora walipata bao dakika ya 77 ya mchezo huo kupitia kiungo wake Morice Chukwu kwa mkwaju wa penati ambaye alitangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kuiwezesha timu yake kupata pointi 3 muhimu.
Pointi hizo zilifanikiwa kuipeleka Tabora nafasi ya 7 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na pointi 11 nyuma ya Mashujaa yenye pointi 12.
Ligi Kuu itaendelea kesho kwa michezo mitatu Singida Black Star dhidi ya Fountain Gate katika Uwanja wa Liti mkoani Singida ,Simba dhidi ya Namungo katika Uwanja wa KMC Dar es Salaam na Azam wataikaribisha Ken Gold katika Uwanja wa Azam Complex.