LIGI Kuu ya NBC iliyo nafasi ya 6 kwa ubora barani Afrika leo inaendelea kwa michezo mitatu itakayochezwa jijini Dar es Salaam na mkoani Singida.
Mchezo wa kwanza utachezwa majira ya saa nane mchana katika Uwanja wa Liti mkoani Singida, ukizikutanisha timu za Singida Black Star na Fountain Gate.
Fountain itawakosa washambuliaji wake wawili muhimu Seleman Mwalimu na Wiliam Edgar ambao wameitwa timu ya taifa ya Tanzania kwa ajili ya michezo ya kufuzu CHAN 2024 dhidi ya Sudan .
Mchezo wa pili utachezwa saa 10 jioni katika Uwanja wa KMC Dar es Salaam ambapo timu ya Simba iliyopo nafasi ya 3 katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na alama 16 itaikaribisha timu ya Namungo kutoka Ruangwa iliyo nafasi ya 13 ikiwa na alama 6.
Mchezo wa tatu utachezwa majira ya saa 1 jioni Azam inayoshika nafasi ya 5 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na alama 15 itakuwa mwenyeji wa timu ya Ken Gold kutokea Mbeya inayoshika nafasi ya 16 kwenye msimamo ikiwa na alama 4.