YANGA YAKWEA KILELENI KWENYE MSIMAMO WA LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Yanga imeendeleza ubabe msimu huu baada ya kushinda mchezo wa nane mfululizo wa Ligi Kuu ya NBC kwa bao moja ugenini dhidi Singida Black Stars.

Bao pekee la Yanga lilifunga na Pacome Zouzoua na kufanya Singida kupoteza mchezo wake wa kwanza msimu huu.

Yanga imecheza mchezo wake wa nane msimu huu bila kuruhusu bao lolote huku ikiwa imefunga jumla ya mabao 13.

Ushindi huo unaifanya Yanga kufikisha jumla ya alama 24 na kuongoza Ligi Kuu ya NBC baada ya kucheza michezo nane.

Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa mchezo mmoja utakaopigwa kwenye uwanja wa KMC, Dar kati ya KMC na Namungo

5 comments

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *