LIGI Kuu ya NBC inatarajiwa kuendelea leo kwenye uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma kwa mchezo kati ya Mashujaa itakayokuwa mwenyeji wa Simba saa 10:00 alasiri.
Mashujaa iliyopoteza mchezo mmoja pekee msimu huu sawa na Simba inashuka uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kupata sare kwenye mchezo wa mwisho dhidi ya Fountain Gate ugenini.
Mashujaa imeshinda michezo mitatu na kutoa sare minne hadi sasa inakutana na Simba iliyoshinda michezo sita ya Ligi Kuu ya NBC na kutoka sare mchezo mmoja pekee.
Simba inahitaji kushinda mchezo wa leo ili kuishusha Singida Black Stars na kupanda hadi nafasi ya pili kwa tofauti ya wastani wa mabao.