AZAM YATAMBA UGENINI ,SINGIDA, COASTAL HAKUNA MBABE

Ligi Kuu ya NBC jana iliendelea kwa michezo miwili iliyochezwa jijini Dar es Salaam katika Uwanja wa Azam Complex na Uwanja wa Amaan Complex visiwani Zanzibar.

Timu ya Yanga ilikuwa mwenyeji wa Azam katika mchezo maarufu kama ‘dabi ya Dar es Salaam’ na kupoteza kwa bao moja huku beki wa Yanga Ibrahim Bacca akishindwa kumaliza mchezo baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia rafu mshambuliaji wa Azam Nassoro Saadun.

Gibril Sillah ndiye aliyefunga bao pekee dakika ya 34 ya mchezo huo uliokuwa na upinzani mkali kwani timu zote zilikuwa zikishambuliana muda wote.

Mchezo wa pili uliochezwa saa mbili na nusu usiku mjini Zanzibar Singida Black Star walishindwa kutamba mbele ya timu ya Coastal Union baada ya kulazimishwa suluhu.

Ligi Kuu ya NBC leo itaendelea jijini Mbeya ambapo Tanzania Prisons watawakaribisha KenGold katika Uwanja wa Sokoine saa 10 alasiri.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *