ILIKUWA WIKIENDI YA KIBABE LIGI KUU NBC

LIGI Kuu ya NBC iliendelea mwishoni mwa wiki iliyopita kwa michezo mitatu iliyochezwa katika mikoa ya Lindi, Kagera na Dar es Salaam.

Namungo iliwakaribisha JKT Tanzania katika mchezo uliochezwa uwanja wa Majaliwa Ruangwa mkoani Lindi katika mchezo uliomalizika kwa suluhu.

Golikipa wa Namungo Jonathan Nahimana alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kufanikiwa kudhibiti mashambulizi yaliyolenga langoni kwake.

Katika mchezo uliochezwa siku ya jumamosi uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera timu ya Kagera Sugar iliikaribisha Simba majira ya saa kumi alasiri.

Simba ndio ilikuwa wa kwanza kutikisa nyavu za Kagera Sugar baada ya beki wa timu hiyo Shomari Kapombe kufunga bao la dakika ya 13 ya mchezo huo na baadae Jean Ahoua aliiongezea timu yake bao dakika ya 44 ya mchezo huo na kuifanya Simba kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao mawili.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi timu zote zikishambuliana na dakika ya 53 ya mchezo huo kiungo wa Simba, Fabrice Ngoma alifunga bao la tatu kwa kichwa baada ya mpira wa kona kupigwa na Ladack Chasambi.

Steven Mukwala aliongeza bao la nne kwa timu ya Simba akipokea pasi kutoka kwa Ladack Chasambi dakika ya 66 ya mchezo huo na Kagera Sugar ilipata bai kupitia Datius Peter dakika ya 79 na Mukwala alirudi tena kambani kwa Kagera dakika ya 84 na dakika chache baadae Cleophace Mkandala wa Kagera aliongeza bao hivyo mchezo kumalizika 2-5.

Kiungo wa Simba Jean Ahoua alitangazwa kuwa nyota wa mchezo huo kutokana na namna alivyoisaidia timu yake kupata ushindi.

Mchezo Mwingine ulichezwa siku ya jumapili katika uwanja wa KMC Complex mkoani Dar es Salaam timu ya Yanga ilikuwa mwenyeji wa Prisons kutoka Mbeya.

Dakika ya 13 ya mchezo huo mshambuliaji wa Yanga Clement Mzize alifungua ukurasa wa mabao na beki wa timu hiyo Ibrahim Hamad aliongeza bao la pili dakika ya 42 ya mchezo huku mshambuliaji Prince Dube akifunga dakika ya 45 hivyo kuifanya Yanga kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 3-0.

Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku Yanga ikishambulia zaidi na dakika ya 83 beki wa timu hiyo Ibrahim Hamad aliongeza bao la nne kwa timu yake hivyo kuifanya mechi kuisha 4-0.

Beki wa Yanga Ibrahim Hamad alitangazwa kuwa nyota wa mchezo huo baada ya kuisaidia timu yake kupata ushindi wa mabao manne huku yeye akifunga mabao mawili katika mchezo huo.

Ligi Kuu ya NBC itaendelea kesho kwa michezo miwili Simba watawakaribisha JKT Tanzania katika uwanja wa KMC huku Singida wakiwakaribisha Kengold uwanja wa CCM Liti.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *