MZIZE,DUBE HAWASHIKIKI LIGI KUU NBC

WASHAMBULIAJI wa Yanga Prince Dube na Clement Mzize wameongeza kasi katika mbio za ufungaji bora baada ya kufung mabao mawili kila mmoja katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya KenGold mchezo uliochezwa leo katika uwanja wa KMC.

Licha ya Kocha Mkuu wa Yanga Saed Ramovic kuaga jana ikiwa ni saa chache kuelekea mechi yao dhidi ya KenGold Yanga imefanikiwa kufunga mabao 6-1 .

Prince Dube ndio alifungua ukurasa wa mabao ikiwa ni dakika ya pili ya mchezo huo kabla ya Mzize  kufunga baola pili dakika ya sita ya mchezo huo huku Pacome Zouzuoa akiongeza bao la tatu dakika ya 39 dakika  nne mbele Mzize alirudi tena na kufunga bao la nne huku Dube akiongeza bao la tano dakika ya 43 y mchezo huo na kuwafanya Yanga kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 5-0.

Kipindi cha pili kilianza huku Yanga wakionekana kuzidi kulisakama lango la kenGold  licha ya timu zote kufanya mabadiliko ya wachezaji  ambapo Yanga dakika ya 85 Duke Abuya aliongeza bao la 6 kwa  timu yake.

KenGold walipata bao la kujifutia machozi kupitia mchezaji wake Seleman Rashid baada ya kupiga mpira mrefu ambao ulimshinda kipa wa Yanga Djigui Diarra hivyo mchezo kutamatika kwa 6-1.

Mshambuliaji wa Yanga Prince Dube alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mechi hiyo baada ya kuonyesha kiwango kizuri katika mchezo huo.

Ligi Kuu itaendelea kesho kwa michezo minne ambapo Dodoma Jiji watawakaribisha Pamba,Tanzania Prisons dhidi ya Mashujaa,Fountain Gate wakiwakaribisha Simba na Azam watacheza na KMC .

2 comments

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *