Tag: #LIGIKUU #NBCPL #AZAM #YANGA #SIMBA #KMC #JKT #MASHUJAA #KENGOLD #DODOMAJIJI #PAMBAJIJI #KAGERASUGAR #SINGIDABLACKSTARS #FOUNTAINGATE #NAMUNGO

MASHUJAA, YOUNG AFRICANS, NAMUNGO, VITANI LEO LIGI KUU YA NBC.

VIWANJA vitatu vya Ligi Kuu NBC vinaendelea kutoa burudani leo kwa ratiba ya michezo mitatu inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku kila timu ikihitaji alama kwa malengo tofauti msimu huu.

Macho mengi yataelekezwa katika viwanja vya Lake Tanganyika, Kigoma, KMC Complex, Dar es Salaam na Majaliwa, Lindi ambako mapambano ya kibingwa yanayohusisha vita ya nafasi za juu pamoja na presha ya kushuka daraja kupamba moto.

Katika mchezo wa mapema utakaochezwa saa 10:00 jioni kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, Mashujaa FC watawakaribisha Pamba Jiji kwenye mechi inayobeba uzito mkubwa kwa timu zote mbili.

Mashujaa wakiwa nyumbani watataka kutumia faida ya mashabiki wao kutafuta ushindi muhimu baada ya kushindwa kupata matokeo mchezo uliopita dhidi ya Fountain Gate huku Pamba Jiji wakisaka matokeo chanya yatakayowaweka kwenye nafasi salama zaidi kwenye msimamo wa ligi.

Mechi hii inatarajiwa kuwa ya nguvu nyingi katikati ya uwanja kutokana na timu zote kupenda kucheza kwa presha huku wakitumia zaidi viungo wa kati kuliko viungo wa pembeni.

Mchezo mwingine mkubwa wa leo utakuwa kati ya Young Africans watakapowakaribisha Tanzania Prisons katika uwanja wa KMC Complex, Dar es Salaam saa 12:30 jioni.

Young Africans wakiwa kwenye mbio za kuwania ubingwa hawana nafasi ya kupoteza alama na ushindi wa leo unaweza kuongeza presha kwa wapinzani wao kwenye kilele cha msimamo.

Tanzania Prisons nao wanakuja na morali ya kutafuta matokeo ya kushtua wakifahamu kupata alama dhidi ya timu kubwa kunaweza kubadili kabisa mwenendo wao wa msimu huu.

Usiku wa leo saa 3:00 usiku timu ya Namungo FC itawakaribisha JKT Tanzania kwenye uwanja wa Majaliwa katika pambano jingine linalosubiriwa kwa hamu.l kukamilisha burudani za siku ya leo.

Namungo wamekuwa timu ngumu sana inapocheza nyumbani jambo linalowapa nguvu dhidi ya JKT Tanzania ambao nao mara nyingi huonekana kuwa na nidhamu kubwa ya kiuchezaji chini ya kocha Ahmad Ally ambaye pia ni kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania.

Hii inaweza kuwa moja ya mechi ngumu zaidi ya leo kutokana na ubora unaokaribiana kwa pande zote mbili.

Kwa ujumla, ratiba ya leo inaweza kuleta mabadiliko makubwa kwenye msimamo wa ligi hasa kwa timu zinazowania ubingwa, nafasi za juu na zile zinazokwepa hatari ya kushuka daraja.

Mashabiki wanatarajia kuona mabao, ushindani mkali na matokeo yatakayoongeza joto la NBC Premier League kuelekea hatua za mwisho za msimu huku kila timu ikitaka kumaliza kwa furaha na mafanikio.

DODOMA JIJI, MBEYA CITY ZAWASHA MOTO LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu NBC imeendelea jana kwa michezo miwili iliyotoa burudani ya viwango ambapo Dodoma Jiji iliichapa Fountain Gate mabao 3-0, huku Mbeya City ikiibuka na ushindi wa kusisimua wa 3-2 dhidi ya KMC.

Katika mchezo uliopigwa Airtel Stadium, Singida, wenyeji Dodoma Jiji walionyesha ubora mkubwa hasa kipindi cha pili na kuondoka na alama tatu muhimu mbele ya Fountain Gate baada ya kipindi cha kwanza kumalizika wakiwa kifua mbele kwa bao moja kupitia kwa nahodha Augustino Nsata aliyefunga dakika ya 38.

Iddi Kipagwile aliongeza bao la pili dakika ya 69 na dakika za nyongeza Yasin Mgaza alihitimisha ushindi huo kwa bao la tatu dakika ya 90+1 na kuifanya Dodoma kushinda kwa kishindo 3-0.

Ushindi huo unaifanya Dodoma kuendelea kuimarisha nafasi yao katikati ya msimamo wa ligi ikikaa nafasi saba ikiwa imekusanya alama 24.

Kwa upande mwingine, katika mchezo uliochezwa Tanzanite Kwaraa, Manyara, mashabiki walishuhudia moja ya mechi tamu zaidi za wiki hii baada ya Mbeya City kuifunga KMC 3-2.

KMC ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Oscar Paul dakika ya 44, na kwenda mapumziko wakiwa mbele.

Kipindi cha pili Mbeya City walibadilika kabisa, wakisawazisha kupitia Riphat Msuya dakika ya 64, kabla ya Adili Buha kufunga kwa penalti dakika ya 76 na kuwapa uongozi wenyeji.

Hata hivyo, KMC hawakukata tamaa na walifanikiwa kusawazisha dakika ya 78 kupitia Juma Shemvuni, jambo lililoongeza presha kubwa kwa wenyeji Mbeya City.

Wakati mchezo ukionekana kuelekea sare, Said Naushad alitokea kuwa shujaa wa Mbeya City kwa kufunga bao la ushindi dakika ya 86, na kuamsha shangwe kubwa Tanzanite Kwaraa. 

Matokeo hayo yana maana kubwa kwenye mbio za msimamo wa ligi, hasa kwa Mbeya City ambao walikuwa wanahitaji sana ushindi huo kujinasua kutoka maeneo ya hatari ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Kwa ujumla, jana ilikuwa siku ya mabao 8 kwenye michezo miwili, ushindi wa kishindo kwa Dodoma Jiji na ushindi wa jasho kwa Mbeya City, matokeo ambayo yanaongeza ushindani mkubwa zaidi msimu huu.

AZAM YAONGEZA PRESHA KWENYE ‘KILELE’ CHA LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Azam imeonyesha ubora na ukomavu mkubwa baada ya kuibuka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Singida Black Stars kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Airtel Stadium, Singida.

Baada ya kutoka sare mbili mfululizo bila kufungana, kikosi hicho cha kocha Florent Ibenge kilirejea kwa nguvu na kuonyesha dhamira ya kupambania nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Bao la kwanza la Azam lilifungwa mapema kipindi cha pili kupitia kwa nahodha Lusajo Mwaikenda aliyemalizia kwa ustadi mpira wa krosi uliotengenezwa na Iddy Seleman ‘Nado’.

Dakika chache baadaye, staa wa timu hiyo Feisal Salum “Fei Toto” aliandika bao la pili kwa shuti la utulivu baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa ‘Nado’ bao ambalo liliongeza presha kubwa kwa wenyeji Singida.

Singida Black Stars walijitahidi kurejea mchezoni na kufanikiwa kupata bao moja kupitia kwa Ayubu Lyanga dakika ya 71, lakini juhudi zao za kusawazisha ziligonga mwamba mbele ya safu imara ya ulinzi ya ‘Matajiri wa chamazi’.

Matokeo hayo yanaifanya Azam kuendelea kuwepo kwenye mbio za ubingwa msimu huu ikikwea hadi nafasi ya pili baada ya kukusanya alama 32 huku ikionyesha kuwa bado ni tishio kubwa kwa vigogo wengine wa ligi, hasa kuelekea ‘duru’ la mwisho la Ligi Kuu ya NBC.

DODOMA JIJI WAJIPATA JAMHURI

Timu ya Dodoma Jiji imejipata katika uwanja wake wa nyumbani wa Jamhuri baada ya kuhakikisha wanashinda kila mchezo wawapo hapo.

Dodoma ambayo imecheza na timu ya TRA United jana imefanikiwa kushinda michezo minne katika uwanja huo,sare mbili na huku ikipoteza mchezo mmoja tu katika michezo saba ambayo timu hiyo imecheza uwanjani hapo.

Mchezaji wa Dodoma Jiji,Dickson Mhilu

Katika mchezo wa jana ulionza majira ya saa moja usiku Dodoma ilionekana ikizitaka alama zote tatu kutoka kwa TRA kwani timu hiyo ilitawala mchezo ambapo dakika ya 15 ya mchezo huo Faraji Kayanda alifungua ukurasa wa mabao.

TRA nayo ilionekana ikiuta ka mchezo kwa kutaka kusawazisha hata hivyo ndoto yao ilizimwa na mchezaji wa Gadiel Michael ambaye aliongeza bao la pili kwa timu yake hivto kwenda mapumziko Dodoma ikiwa mbele kwa mabao mawili.

Kipindi cha pili kilirejea ambapo dakika ya 55 Edgar William alizidi kudidimiza matumaini ya TRA baada ya kuongeza bao la tatu kwa timu yake ambapo mpaka mchezo unatamatika Dodoma iliibuka na ushindi wa 3-0 hivyo timu hiyo ilipanda kutoka nafasi ya saba hadi ya sdita katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.
[13/02/2026, 09:26:53] Honest Tplb: mkuu

YOUNG AFRICANS YAREJEA KILELENI LIGI KUU YA NBC.

TIMU ya Young Africans imeendelea kuonyesha kwanini inaiwakilisha nchi kwenye mashindano ya Afrika baada ya kushinda 3-1 dhidi ya Dodoma Jiji na kukwea hadi nafasi ya kwanza ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

Young Africans iliyokuwa ya kwanza kuruhusu bao dakika nne kabla ya kipindi cha kwanza kutamatika kupitia kwa Edgar William haikukata tamaa na zikisalia dakika tatu mchezo kwenda mapumziko ilisawazisha kupitia kwa Laurindo Dilson akitumia mkwaju wa penati baada ya Andy Bikoko kumchezea rafu mchezaji wa Young Africans.

Kipindi cha pili Laurindo aliongeza bao na Prince Dube kupigilia msumari wa tatu na kupeleka furaha kwa ‘Wananchi’ na huzuni kwa ‘wakulima wa zabibu’.

Laurindo Dilson ‘Depu’ amekuwa na kiwango bora kwenye Ligi Kuu ya NBC tangu ajiunge na Young Africans akifunga mabao matatu na kutoa pasi ya bao moja huku akishinda tuzo ya mchezaji bora wa mchezo dhidi ya Dodoma Jiji na kufanikiwa kuifanya Young Africans kurejea kileleni ikifikisha jumla ya alama 22.

Young Africans inaungana na Azam Fc na kuwa timu pekee ambazo hazijapoteza mchezo hadi sasa kwenye Ligi Kuu ya NBC na zikiwa zimeruhusu mabao machache pia (2) huku ‘Wananchi’ wakiongoza kwa kufunga mabao hadi sasa (21).

Mkoani Tanga kwenye uwanja wa Mkwakwani Coastal Union ililazimishwa sare ya bao moja na timu ya KMC ikiwa sare ya pili kwa KMC iliyopoteza michezo nane hadi sasa na ikishika nafasi ya mwisho ya msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.

KMC iliyoshinda mchezo mmoja pekee hadi sasa imefanikiwa kufikisha mabao matatu kwenye ligi hiyo ikiwa timu iliyofunga mabao machache hadi sasa huku ikiongoza kwa kufungwa mabao mengi (18).

Sare hiyo inaifanya Coastal Union iliyopoteza mchezo wao uliopita ugenini dhidi ya Namungo kukwea hadi nafasi ya 11 ikifikisha jumla ya alama 10 ikiwa imepata ushindi kwenye michezo miwili pekee.