LIGI Kuu ya NBC inatarajiwa kuendelea leo kwa mchezo mmoja utakaozikutanisha timu za Simba dhidi ya Dodoma kwenye uwanja wa KMC Complex, Dar.
Simba iliyoshinda mchezo wake wa Ligi Kuu ya NBC uliopita ugenini dhidi ya Coastal Union kwa mabao 3-0 inakutana na Dodoma Jiji iliyolazimishawa suluhu na Coastal kwenye uwanja wa Jamhuri, Dodoma.
Timu ya Simba inahitaji alama tatu leo ili kujiweka nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa NBC msimu huu huku Dodoma ikihitaji kupata ushindi ili kujihakikishia nafasi ya kusalia kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26.
Mchezo huu ni wa kiporo ulioahirishwa baada ya timu ya Dodoma Jiji kupata ajali ya basi ilipokuwa ikitoka mkoani Lindi baada ya mchezo dhidi ya Namungo kwenye uwanja wa Majaliwa, Lindi.