FEISAL MKALI WA ‘KUPIKA MABAO’ LIGI KUU YA NBC

KIUNGO wa Azam,Feisal Salum ameendelea kuwa kinara wa kupika mabao katika Ligi Kuu ya NBC kutokana na kuweza kutoa pasi 12 za mwisho kwa msimu wa 2024/2025 katika michezo 23 ambayo timu yake imeshacheza mpaka sasa akivunja rekodi ya msimu uliopita ambapo  Kipre Junior alimaliza na asisti 9.

Feisal ametoa pasi za mwisho katika michezo ya Azam dhidi za Namungo (1),JKT Tanzania (2),Fountain Gate (1),Coastal Union (1),Simba dhidi ya Azam (1),Azam dhidi ya KMC (1)  Tabora dhidi ya Azam (1).

Mechi zingine ambazo Feitoto ameweza kutoa pasi za mwishi ni  Dodoma Jiji dhidi ya Azam (1), Namungo dhidi ya Azam (1), KMC dhidi ya Azam (2).

Ukiachana na Feisal wachezaji Jean Ahoua wa Simba,Max Nzegeli ,Aziz Ki na Prince Dube wa Young Africans wamefanikiwa kutoa pasi za mwisho  saba kila mmoja.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *