‘TSHABALALA’ MKALI WA PASI ZA MWISHO LIGI KUU NBC.

BEKI wa timu ya Simba,Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ ndiye kinara wa  kutoa pasi za mwisho kwenye Ligi Kuu ya NBC msimu huu wa 2024/2025 akiwa nazo nne.

Tshabalala alitoa pasi za mwisho na kuisaidia timu yake kupata alama katika michezo ya Simba dhidi ya timu za Fountain Gate (1),Dodoma Jiji (1),Tabora (1) na Kagera Sugar.

Nafasi ya pili inashikiliwa na beki wa Singida Black Stars, Ande Koffi akiwa ametoa pasi tatu katika mechi za Singida dhidi ya Fountain Gate (1),Pamba Jiji (1) na KenGold (1).

Datius Peter wa Kagera Sugar anafuata akiwa na pasi za mwisho tatu alizotoa katika michezo ya Kagera Sugar dhidi ya timu za Pamba Jiji (1),KenGold (1) na mchezo wa Mashujaa (1).

Beki wa Simba, Shomari Kapombe, amepiga pasi za mwisho tatu alizoweza kutoka katika michezo ya timu yake dhidi ya Prisons (2) na Fountain Gate (1).

Beki na nahodha wa Fountain Gate,Amos Kadikilo anashika nafasi ya tano akiwa na pasi za mwisho tatu alizopata katika michezo ya Fountain Gate dhidi ya Namungo (1) na Tanzania Prisons (2).

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *