NANI kuungana na Hausung kwenye Ligi ya Championship ya NBC ndiyo swali linalosubiri majibu yake kutoka kundi B la First League ambapo Rhino Rangers, Gunners na Tanesco wanayo nafasi ya kufanya hivyo.
Rhino Rangers ya Tabora ina Jumla ya alama 31 kwenye michezo 13 huku Gunners ya Dodoma ikiwa na alama 29 kwenye michezo 12 wakati Tanesco ya Morogoro ikiwa na alama 26 kwenye michezo 26.
Ikumbukwe kuwa timu inayoshika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa First League Kundi A na B Inafuzu moja kwa moja kushiriki Ligi ya Championship ya NBC.
Wakati timu zinazoshika nafasi ya pili na ya tatu kwenye kila kundi zikicheza michezo ya mtoano (PlayOff) kupata washindi wawili wa kucheza mtoano wa kupanda (Promotion PlayOff) na timu mbili za ligi ya Championship ya NBC.
GUNNERS FC 💪💪💪