LADHA za Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika zinarejea rasmi leo kwa michezo minne itakayopigwa kwenye viwanja tofauti nchini ikiwa ni baada ya mapumziko ya michuano ya kufuzu Kombe la Dunia 2026.
Mchezo wa kwanza utakuwa jijini Mwanza ambapo timu ya Pamba Jiji itakuwa mwenyeji wa timu ya Namungo katika uwanja wa CCM Kirumba majira ya saa nane mchana.
KMC itacheza dhidi ya timu ya Tanzania Prisons katika uwanja wa KMC Complex uliopo mkoani Dar es Salaam huku Tabora United itakuwa mwenyeji wa Young Africans katika uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora na mchezo wa mwisho utakuwa kati ya Fountain Gate itakayoialika Singida Black Stars katika uwanja wa Tanzanite Kwaraa mkoani Manyara huku michezo yote mitatu ikichezwa saa 10:15 alasiri.