MBEYA STAND NBC CHAMPIONSHIP

MBEYA, STAND VITA YA NAFASI NBC CHAMPIONSHIP LEO.

‘VITA YA NAFASI’ ndivyo unavyoweza kuuita mchezo huu ambapo MBEYA City itaikaribisha Stand United kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya kuanzia saa 10:00 alasiri, kwenye muendelezo wa michezo ya  Ligi ya Championship ya NBC.

Mbeya City ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC ikiwa na alama 52 sawa na Stand United iliyo nafasi ya tatu zikitofautiana kwenye mabao ya kufunga na kufungwa, timu yeyote itakayoshinda mchezo huu itajichukulia kijiti cha nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi hiyo.

MChezo wa mwisho kwa leo utachezwa mkoani Mtwara ambapo Mbeya kwanza ya mkoani hapo itaialika Transit Camp ya Dar es Salaam kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona saa 10:00 alasiri.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *