FAINALI YA FIRST LEAGUE KUPIGWA LEO CHAMANZI.

 

MCHEZO wa Fainali wa Ligi ya First League unapigwa leo April 5 kwenye uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam ukizikutanisha timu za Hausung kutoka Njombe na Gunners ya Dodoma.

Hii inafanyika kwa mara ya kwanza tangu maboresho ya kanuni ya First League kufanyika kwa msimu 2024/25 ambapo hapo awali Bingwa alikuwa akipatikana kwa timu nne za juu kila kundi kucheza shindano dogo la nane bora na timu zikipangwa kwenye makundi mawili yenye jumla ya timu nne na vinara wa kila kundi hucheza mchezo wa nusu fainali na fainali na hatimaye Bingwa kupatikana.

Ikumbukwe kuwa timu hizi tayari zimekwisha kata tiketi ya moja kwa moja kushiriki Ligi ya Championship ya NBC kwa msimu wa 2025/2026 kwa kuongoza makundi yao.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *