TIMU ya Kagera Sugar imeanza kujipata katika michezo ya Ligi Kuu ya NBC baada ya kushinda mechi tatu walizocheza hivi karibuni chini ya uongozi wa Kocha wao mpya Juma Kaseja ambaye pia ni golikipa aliyecheza kwa mafanikio makubwa timu ya taifa na timu mbalimbali za Ligi Kuu .
Kaseja ambae alichukua mikoba kutoka kwa Kocha Melis Medo ambae ametimkia katika timu ya Singida Black Stars aliiongoza timu yake katika mchezo miwili huku mchezo wa kwanza dhidi ya Pamba Jiji alifanikiwa kushinda mabao 2-1.
Mchezo mwingine ulichezwa jana April 3 alifanikiwa kuifunga timu ya Coastal Union kwa mabao 2-1 ambapo mabao ya Kagera Sugar yalifungwa na Ally Msangi wa Coastal Union aliyejifunga bao dakika ya 59 na Mohamed Jecha dakika ya 90 huku mchezaji Lucas Kikoti akiipatia Coastal Union bao dakika ya 84 ya mchezo huo.
Kagera Sugar imefikisha alama 22 ikiwa nafasi ya 14 kwenye msimamo baada ya kucheza michezo 24 wakifunga mabao 20 na kufungwa mabao 32.