TIMU ya Gunners kutoka mkoani Dodoma imefanikiwa kuwa Bingwa wa First League msimu wa 2024/2025 baada ya kuifunga Hausung mabao 3-0 kwenye mchezo wa Fainali uliochezwa jana Azam Complex, Dar es salaam.
Gunners ilimaliza kinara wa Kundi B ikiwa na alama 35 kwenye michezo 14 hivyo kupata nafasi ya kucheza mchezo wa Fainali ulioipa timu hiyo ubingwa.
Kwa upande wa Hausung ilimaliza kinara wa kundi A ikiwa na alama 25 kwenye michezo 14, alama ambazo ziliipa timu hiyo nafasi ya kucheza mchezo huo wa fainali kumtafuta bingwa wa jumla wa First League 2024/2025.
Timu zote mbili zimekata tiketi ya kushiriki Ligi ya Championship ya NBC msimu wa 2024/2025 baada ya kumaliza vinara wa makundi yao.