LIGI Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja uliochezwa uwanja wa KMC Complex ambapo timu ya Young Africans iliikaribisha timu ya Coastal Union kutoka Tanga.
Mchezo huo ulianza majira ya saa kumi na robo jioni ambapo timu zote zilikuwa zikishambuliana huku pia zikiimarisha ulinzi katika lango lao ili kutokuruhusu bao lolote.
Ilimchukua dakika 34 mchezaji wa Young Africans Pacome Zouzoua kufungua ukurasa wa mabao hivyo kuifanya timu yake kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao moja.
Kipindi cha pili kilianza ambapo timu zote zilionekana zikitaka alama tatu muhimu ambapo hata hivyo mchezo ulitamatika kwa Young Africans kuibuka na ushindi wa bao 1-0.
Youn Africans imezidi kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwania ubingwa baada ya kufikisha alama 64 huku wakiwa wamecheza michezo 24 na wakiendelea kuongoza katika msimamo wa Ligi Kuu huku timu ya Coastal Union ipo nafasi ya13 katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 25.
PACOME, ni fundi hakuna wa kufanana katika ligi yabongo ya NBC