PAMBA JIJI YABANWA NYUMBANI LIGI KUU YA NBC.

Ligi Kuu ya NBC imeendelea kwa mchezo mmoja uliozikutanisha Pamba jiji na Fountain Gate kwenye uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza majira ya saa kumi Alasiri.

Kipindi cha kwanza kilianza kwa kasi na dakika ya 22 Mathew Momanyi wa Pamba Jiji alipatia timu yake bao la kwanza kwa mkwaju wa Penati


Dakika ya 61 kipindi cha pili Fountain Gate walifanikiwa kujipatia bao la kusawazisha lililofungwa na Elie Makono na kufanya matokeo kuwa 1-1 na dakika za nyongeza Pamba ilipata mkwaju wa penati na kukoswa na Mathew Momanyi aliyepiga na mpira kugonga mwamba hivyo kufanya mchezo kumalizika kwa matokeo ya 1-1.

Matokeo hayo yanaifanya Pamba jiji kushika nafasi ya 10 na alama 27 huku Fountain Gate ikiwa nafasi ya  8 na alama 29 kibindoni.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *