LIGI ya NBC Champioship inaendelea kushika kasi ikielekea mwishoni na hapo kesho michezo nane ya mzunguko wa 28 itachezwa katika viwanja mbalimbali nchini majira ya saa kumi jioni .
Timu ya Cosmopolitan ambayo iko nafasi ya 13 kwenye msimamo wa Ligi ya Championship ya NBC itaikaribisha timu ya Stand United iliyopo nafasi ya tatu kwenye msimamo katika uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro.
Green Warriors iliyopo nafasi ya 11 kwenye msimamo wa Ligi ya Champioship itaikaribisha timu ya Biashara United ambayo ipo nafasi ya mwisho kwenye msimamo mchezo utakaochezwa uwanja wa Azam Complex Dar es Salaam.
Transit Camp ikiwa kwenye nafasi ya 14 katika msimamo itaikaribisha timu ya TMA iliyopo nafasi ya tano kwenye msimamo mchezo utakaochezwa katika uwanja wa TFF Centre uliopo Kigamboni mkoani Dar es Salaam.
Timu ya Kiluvya iliyopo nafasi ya 12 itaikaribisha timu ya Mbuni ambayo iko nafasi ya tisa katika mchezo utakaochezwa uwanja wa Mabatini mkoani Pwani.
Mbeya Kwanza iliyo nafasi ya sita itachuana vikali na African Sports iliyo nafasi ya 15 mchezo utakaochezwa uwanja wa Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara.
Timu ya Bigman iliyo nafasi ya saba itawaalika timu ya Mtibwa Sugar inayoongoza Ligi ya Championship ya NBC katika uwanja wa Ilulu mkoani Lindi.
Wachimba madini yaani Geita Gold iliyo nafasi ya nne kwenye msimamo itawakaribisha Mbeya City iliyo nafasi ya pili katika uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita huku Songea United iliyopo nafasi ya nane ikiwakaribisha Polisi Tanzania iliyo nafasi ta 10 katika uwanja wa Majimaji mkoani Songea.