LIGI KUU YA NBC KUREJEA MEI 2

LIGI Kuu ya NBC, Ligi namba nne kwa ubora barani Afrika  itarejea Mei 2 kwa mchezo kati ya Simba itakayokuwa mwenyeji wa timu ya Mashujaa kutoka mkoani Kigoma.

Mchezo huo utachezwa katika uwanja wa KMC Complex uliopo mkoani Dar es Salaam ikiwa ni mchezo wa mzunguko wa 24 uliosogezwa kutokana na timu ya Simba kuwa na ratiba ya michezo ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Baada ya mchezo huo timu ya Simba itakuwa na kibarua kingine ugenini katika uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar watakapokutana na timu ya JKT Tanzania waliyoifunga 1-0 kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza kwa bao la Jean Ahoua aliefunga kwa mkwaju wa penati dakika za nyongeza.

Mei 8 itaikaribisha timu ya Pamba katika uwanja wa KMC Complex kabla ya kwenda ugenini kuvaana na timu ya KMC kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *