SIMBA, SINGIDA BS KINAPIGWA LIGI KUU NBC LEO.

LIGI Kuu ya NBC inaendelea leo Mei 28 kwa mchezo mmoja wa kukamilisha mzunguko wa 28 Kati ya Simba na Singida Black Stars katika uwanja wa KMC, Dar es Salaam.

Katika mchezo wa mwisho timu hizo kukutana mkoani Singida timu ya Singida ilikubali kichapo cha bao 0-1 mbele ya Simba kwenye uwanja wake wa Nyumbani CCM Liti bao likifungwa na Fabrice Ngoma.

Simba inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa na alama 69 ikishinda michezo 22 ikitoka sare michezo mitatu na kupoteza mchezo mmoja pekee.

Singida Black Stars ipo nafasi ya 4 kwenye msimamo ikiwa na alama 53 baada ya kushinda michezo 16 ikitoka sare mitano na kupoteza michezo sita.

2 comments

Join the Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *