HATMA ya kucheza mchezo wa mtoano kushiriki Ligi Kuu ya NBC kujulikana leo ambapo timu ya Stand United itakuwa mwenyeji wa Geita Gold kwenye uwanja wa CCM kambarage, Shinyanga saa 10:00 alasiri.
Mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye uwanja wa Nyankumbu ulimalizika kwa Sare ya mabao 2-2 hivyo kuufanya mchezo wa leo kuwa mgumu zaidi timu zote zikitafuta nafasi ya kucheza Ligi Kuu ya NBC.
Ushindi, suluhu au sare ya bao 1-1 unaipa nafasi Stand United kusonga mbele kwenye mchezo wa mtoano unaofuata kwa Faida ya mabao ya ugenini.
Ushindi au sare ya mabao 3-3 na kuendelea unaipa Geita Gold nafasi ya kuendelea kwenye mchezo wa mtoano unaofuata kwa faida ya mabao mengi ya ugenini.
Mshindi wa jumla wa michezo hii ya mtoano wa kupanda (Promotions Playoffs) atacheza na timu iliyofungwa kwenye mchezo wa mtoano utakaozikutaisha timu iliyoshika nafasi ya 13 na 14 kwenye Ligi Kuu ya NBC.