YOUNG AFRICANS, SIMBA ‘HAWAFUNGIKI’ UGENINI LIGI KUU YA NBC.

KLABU za Simba na Young africans ni timu pekee za Ligi Kuu ya NBC ambazo hazijafungwa kwenye mchezo wowote wa ugenini msimu huu zikicheza michezo 27 kila moja.

Young Africans katika msimu huu wa Ligi Kuu imefanikiwa kucheza michezo 14 viwanja vya ugenini na kufanikiwa kushinda michezo 13 huku ikipata sare moja na ikivuna alama 40 ikiweka ‘kimiani’ mabao 35 na kuruhusu mabao mawili pekee.

Kwa upande wa timu ya Simba imefanikiwa kucheza michezo 13 ugenini ikishinda michezo 12, sare moja na kuvuna alama 37 baada ya kufunga mabao 25 na kuruhusu mabao manne pekee.

Ligi Kuu ya NBC itaendelea juni 15 kwa mchezo wa dabi ya Kariakoo ambapo timu ya Young Africans itakuwa mwenyeji wa timu ya Simba katika uwanja wa Benjamin Mkapa mkoani Dar es Salaam saa 11:00 jioni.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *