‘WAGOSI wa kaya’ timu ya Coastal Union imefanikiwa kupanda ushindi wa tatu mfululizo kwenye uwanja wake wa Mkwakwani tangu kukamilika marekebisho yake baada ya kuifunga timu ya Fountain Gate 1-0.
Lucas Kikoti ndiye aliyepeleka furaha kwa wakazi wa mkoa wa Tanga akifunga kwa mkwaju wa penati uliopatikana kipindi cha pili.
Tangu uwanja huo urejeshwe kwenye matumizi Coastal imezifunga timu za Singida Black Stars kwa mabao 2-1, Ken Gold 2-1 na ushindi wa jana unakamilisha mchezo wa tatu mfululizo wakitumia uwanja huo wakiwa hawajapoteza wala kutoa sare.
Coastal imefikisha alama 34 na kujihakikishia nafasi ya kushiriki Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/26 huku ikisalia na mchezo mmoja kukamilisha msimu.
Bakari Msimu wa Coastal Union aliibuka mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kuonyesha kiwango bora zaidi ya wachezaji wenzake.