TIMU ya Tanzania Prisons imeshindwa kuonyesha ubabe ikicheza uwanja wa nyumbani wa Sokoine, Mbeya baada ya kukubali kipigo cha mabao 0-5 kutoka kwa Young Africans.
Ilimchukua dakika 31 Mudathir Yahya kuiandikia Young Africans bao la kuongoza kabla ya dakika tatu baadae Clatous Chama kuongeza msumari wa pili na kuwafanya ‘Wananchi’ kwenda mapumziko wakiongoza mabao 0-2.
Dakika 11 baada ya kipindi cha pili kuanza Pacome Zouzoua aliongeza ‘chuma’ cha tatu huku dakika nne baadae Israel Mwenda akaongeza la nne kwa kichwa baada ya kuunganisha mpira wa krosi ya Chadrack Boka na dakika ya 75 Pacome aliingia kambani tena na kukamilisha karamu ya mabao kwa Young Africans.
‘Wananchi’ wameendelea kujikita kileleni baada ya ushindi huo wakifikisha alama 76 huku wakiwa wamefunga mabao 76 wakifuatiwa na timu ya Simba yenye alama 75 wakifunga mabao 68 huku timu hizo zikisalia na michezo miwili kutamatisha msimu wa Ligi Kuu ya NBC.
Pacome Zouzoua aliibuka nyota wa mchezo na kukabidhiwa tuzo ya mchezaji bora wa mechi akifunga mabao mawili na kuisaidia timu yake kupata alama tatu.
pleas naomben saport
saport zenu zatosha