MZUNGUKO wa tatu wa Ligi Kuu ya NBC unaendelea leo mkoani Dar es salaam katika viwanja viwili vya Meja Jenerali Isamuhyo na uwanja wa Benjamin Mkapa.
Katika mchezo wa kwanza utakaochezwa Isamuhyo majira ya saa kumi na mbili jioni timu ya JKT Tanzania inayonolewa na kocha Ahmad Ally itakuwa mwenyeji wa Azam iliyo chini ya Florent Ibenge.

JKT inashika nafasi ya nne katika msimamo wa Ligi Kuu ya NBC ikiwa imekusanya alama nne baada ya kushinda mchezo mmoja dhidi ya Coastal Union na kutoka sare na Mashujaa huku timu ya Azam ikishika nafasi ya tisa baada ya kukusanya alama tatu kwenye mchezo mmoja iliyocheza dhidi ya Mbeya City.
Mchezo wa pili ni kati ya Simba na Namungo utakaopigwa majira ya saa 2:15 usiku ukiwa ni mchezo wa mwisho wa kukamilisha mzunguko wa tatu.

Simba iliyo chini ya kocha Selemani Matola inashika nafasi ya nane katika msimamo ikikusanya alama tatu katika mchezo wao pekee waliocheza dhidi ya Fountain Gate.

Namungo ambayo haijapoteza mchezo wowote hadi sasa chini ya kocha Juma Mgunda inakamata nafasi ya tano ikiwa na alama nne baada ya kutoka sare na timu ya Pamba Jiji huku ikiifunga timu ya Tanzania Prisons.
namungu amejaa kwenye mfumo wa MATORA.UBAYA UBWELAAA!!!
namungo wamejaa kwenye mfumo wa MATORA.UBAYA UBWELAAA!!!
Leo ushindi lazima, refa ni wa simbaa..
Ubaya ubwela
Ubora wa ligi unakua kwa kasi sana