TIMU za Geita Gold na Kagera Sugar zimerejea rasmi Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2026/2027 baada ya kufikisha alama ambazo hazitaweza kufikiwa na timu zingine katika michezo ya Ligi ya Championship ya NBC iliyosalia.
Geita Gold imefikisha alama 71 baada ya kuifunga Songea United mabao 3-1 katika mchezo uliochezwa leo na kufanikiwa kurejea Ligi Kuu baada ya takribani misimu miwili wakiwa NBC Championship.
Kagera Sugar imerejea Ligi Kuu baada ya kufikisha alama 68 kwa kuifunga timu ya Ken Gold 3-0 ikiwa ni msimu mmoja tu tangu timu hiyo iliposhuka daraja .
Mbeya Kwanza inayowania kucheza Play off imeifunga Stand United 1-0 huku Bigman ikiifunga timu ya Gunners 2-0.
Barberian imekubali kichapo cha 0-1 kutoka kwa B19 huku Hausung nayo ikipokea kichapo cha 0-1 kutoka kwa Transit Camp.
TMA imaishushia kichapo cha 2-0 timu ya African Sports huku Mbuni ikiifunga 1-0 Polisi Tanzania kwenye mchezo uliokuwa mkali na wa kusisimua.