MZUNGUKO WA 28 NBC CHAMPIONSHIP KUTOA TASWIRA NZIMA LEO

MZUNGUKO wa 28 wa Ligi ya Championship ya NBC unaendelea leo katika viwanja nane nchini ambapo michezo hiyo itachezwa saa kumi alasiri huku michezo miwili ikiwa mbashara kwenye chaneli ya Ligi Kuu Tv inayopatikana Youtube na Fifa+.

Geita Gold itaikaribisha timu ya Songea United katika uwanja wa Nyankumbu mkoani Geita ambapo pia timu ya Geita Gold ikishinda mchezo huo itakata tiketi ya moja kwa moja kupanda Ligi Kuu ya NBC na mchezo huo utakuwa mbashara chaneli ya Ligi Kuu TV katika mtandao wa Youtube.

Mchezo wa pili ni kati ya Kagera Sugar dhidi ya Ken Gold katika uwanja wa Kaitaba mkoani Kagera huku Bigman ikiikaribisha timu ya Gunners kwenye uwanja wa Ilulu mkoani Lindi.

Mbeya Kwanza itakuwa mwenyeji wa Stand United kwenye uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora huku Hausung ikichuana na Transit Camp katika uwanja wa Amani mkoani Njombe.

Timu ya Barberian itakuwa mwenyeji wa timu ya B19 katika uwanja wa Filbert Bayi mkoani Pwani huku mchezo huo ukioneshwa mbashara kupitia Fifa +.

Kwa upande wa Mbuni itaikaribisha timu ya Polisi Tanzania katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha huku TMA ikichuana na African Sports katika uwanja wa Usharika mkoani Kilimanjaro.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *