WACHEZAJI wa timu ya Azam, Iddi Selemani na Feisal Salum, wanashikilia usukani kwenye orodha ya wachezaji waliofunga mabao mengi kwa kutumia mguu wa kulia katika Ligi Kuu ya NBC msimu wa 2025/2026 hadi sasa baada ya kila mmoja kufunga mabao nane.
Nyota hao wa Azam wamekuwa na mchango mkubwa katika safu ya ushambuliaji ya timu yao, wakionyesha umakini mkubwa mbele ya lango na uwezo wa kutumia mguu wao wa kulia kuipa timu yao alama muhimu katika mechi mbalimbali za ligi.
Nyuma yao kuna Ndumumwe Mossi wa Singida Black Stars pamoja na wachezaji wa Young Africans, Mudathir Yahya na Pacome Zouzoua ambao wote wamefunga mabao saba kwa mguu wa kulia.
Orodha hiyo pia inamjumuisha mshambuliaji wa Coastal union, Maabad Maabad ambaye ameweka kambani mabao saba kwa kutumia mguu wa kulia huku akithibitisha kuwa ni mmoja wa washambuliaji hatari wa kuchungwa katika ligi msimu huu.
Takwimu hizi zinaonyesha ushindani mkubwa uliopo miongoni mwa wafungaji wa Ligi Kuu ya NBC, huku vita ya kuwania tuzo mbalimbali za ufungaji ikiendelea kushika kasi kadri msimu unavyoelekea ukingoni.