MBEYA CITY YAJIPATA, AZAM YAILIZA PAMBA JIJI LIGI KUU YA NBC.

LIGI Kuu ya NBC imeendelea kushika kasi ikiwa ni mzunguko wa tatu wa ligi hiyo ambapo timu ya Mbeya City ilikuwa mwenyeji wa timu ya Mashujaa huku Azam ikiikaribisha timu ya Pamba Jiji.

Mchezo wa kwanza ulikuwa katika uwanja wa Sokoine ambapo mwenyeji Mbeya City aliikaribisha Mashujaa kwa kasi kubwa ikiwa kila timu ilikuwa ikizitaka alama tatu muhimu ili kujiweka katika nafasi nzuri kwenye msimamo wa Ligi Kuu huku timu hizo zikienda mapumziko bila kufungana mabao.

Kipindi cha pili kilirejea na timu zote zilikuwa zikionyesha ushindani ambapo iliwachukua dakika 52 timu ya Mashujaa kufungua ukurasa wa mabao kupitia mchezaji wao Hijjah Shamte huku Adilly Buha wa Mbeya City akisawazisha kupitia mkwaju wa penati na dakika ya 79 na Oscar Mwajanga aliiongezea bao la pili timu ya Mbeya City hivyo mchezo kuisha kwa 2-1.

Mchezaji wa Mbeya City Ismail Aziz alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo kutokana na kiwangzzo kizuri alichoonyesha.

Mchezo wa pili ulichezwa majira ya saa moja jioni katika Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam ambapo mwenyeji timu ya Azam aliikaribisha timu ya Pamba Jiji.

Mchezo ulianza kwa timu zote kucheza kwa tahadhari kubwa ili kuhakikisha hazipotezi alama ambapo iliwachukua dakika 24 timu ya Azam kufunga bao la kwanza kupitia mchezaji wao Enock Molia huku Pamba jiji ikisawazisha dakika ya 45 ya mchezo huo kupitia mchezaji wao Nonyem Okorocha na timu hizo zilienda mapumziko 1-1.

Kipindi cha pili kilirejea na mchezaji wa Azam, Abdul Suleiman alifunga bao la pili kupitia mkwaju wa penati baada ya Iddi Seleman kuchezewa madhambi na mchezaji wa Pamba Jiji na mchezo ulitamatika kwa 2-1 mchezaji wa Azam Iddy Seleman alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo.

Start a Conversation

Your email address will not be published. Required fields are marked *