Timu ya Mbeya City imemaliza uteja wake wa kupoteza mechi dhidi ya Namungo kwa kuifunga mabao 2-1 na kupanda nafasi nne za juu katika msimamo wa Ligi Kuu NBC
Mchezo huo wa tano kwa Mbeya city wakicheza katika uwanja wa nyumbani ulishuhudia mabao ya timu hiyo yakifungwa na Sixtus Sabilo na Hassan Muhamud huku bao pekee la Namungo likifungwa na Reliants Lusajo akifikisha mabao sita na kuwa kinara wa wafungaji katika Ligi ya NBC
Matokeo hayo yanaifanya Mbeya City kufikisha alama 15 baada ya mechi tisa huku Namungo wakisalia na alama 15 baada ya kucheza mechi 10
Mchezo huo ulishuhudiwa ukimalizika Dakika zote 90 bila mchezaji yeyote kuonyeshwa kadi ya njano wala nyekundu
Ligi hiyo itaendelea tena Novemba 6 kwa mchezo kati ya Polisi Tanzania dhidi ya Singida Big Stars katika uwanja wa Black Rhino Academy uliopo Karatu mkoani Arusha .